Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Poul Makonda akiongea na umati wa madereva na wapiga debe waliofurika ndani ya kituo cha mabasi Ubungo mapema leo ambapo amewataka madereva kuacha mgomo na waendelee na safari huku matatizo yao ya msingi yakishughulikiwa ikiwemo kuangalia tume iliyoundwa kama imezingatia vitu muhimu akiwemo muakilishi wa madereva anayeaminika pamoja na tume hiyo kuwa ya uwazi huku akisisitiza kuwa, endapo hadi kesho saa nne asubuhi ( Mei 6), tume hiyo haitakuwa na vitu vya msingi, basi amewataka madereva kugoma tema na atawaunga mkono.
Na Andrew Chale, Modewji blog
Mgomo uliodumu zaidi ya masaa 30, hatimaye leo Mei 5, majira ya Saa sita mchana umemalizika na madereva kuingia kwenye magari yao na kuanza safari kufuatia Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Poul Makonda kujitoa kafara kwa kuakikisha atasimamia madai yao yote muhimu yanashughulikiwa kupitia tume iliyoundwa ndani ya masaa 19, huku akiwataka viongozi wa madereva hao kuwa, hadi saa nne kesho endapo mambo hayatotimizwa basi wafanye mgomo upya.
Makonda alieleza kuwa, suala la tume ilioundwa na Waziri Mkuu ya watu 13, kuzingatia mataakwa muhimu na ya msingi kwa madereva ambapo aliwaeleza kuwa tume muhimu itahakikisha inashughulikia madai yao kwa muda wa siku 7 na kutoa majibu.
Akiongea kwa kujiamini, Makonda aliwatangazia madereva haao wote kukiakikisha hadi ifikapo kesho Mei 6, saa nne wawe wamejua haki zao za msingi zimetekelezwa na kuzingatia ikiwemo kamati yao kuwa na mtu wanae mtambua na kumuamini na pia tume hiyo iwe na habibu rejea na muelekeo wa ukomo wake katika utekelezaji majukumu.
“HADI KESHO SAA NNE ASUBUHI!!!! Endapo tume hiyo iliyoundwa haina mtu muhimu wa madereva na munayemjua nyie kuwa hawezi kutatua matatizo yenu munayodai, basi MUGOME NA MIMI NAWAUNGA MKONO TENA NAWAAMBIENI WANANCHI, KESHO MISIKATE TIKETI MUKIONA HALI HAIJAWA SAWA KAMA MAMBO YAO MADEREVA HAWAJATEKELEZEWA!” Alieleza Makonda na kushangiliwa na umati huo wa madereva na wapiga debe.
Pia Makonda alilitaaka jeshi la Polisi kutowasumbua kwa mabomu na mbwa katika shughuli zao ikiwemo mgomo ambapo amewataka kukaa mbali na madereva hao kwani nao wanadai haki zao za msingi.
Mwandishi Mwandamizi wa Modewji blog, Andrew Chale, akiendelea kuchukua matukio moja kwa moja..hatua kwa hatua wakati Makonda anaongea.
Mbunge wa Hai, Moshi na Mkuu wa Kambi ya Upinzani Bungeni na ambaye ni kiongozi mkuu wa UKAWA, Freeman Mbowe, akiongea machache katika mkutano huo. Hata hivyo, Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Poul Makonda alishuka na kipaza sauti na kutokomea nacho hali iliyozua tafrani kwa baadhi ya madereva ambapo hata hivyo Mbowe alizungumza na madereva hao bila kutumia kipaza sauti huku akishangiliwa muda wote. Mbowe alifika Ubungo majira ya saa tano asubuhi na kushangiliwa na umati mkubwa wa madereva hao.
Vijana wapiga debe. wakishangilia basi lililokuwa likitoka ndani ya kituo cha mabasi Ubungo kuelekea Mikoani
Umati wa watu ukiwa nje ukiangalia mabasi yaliyokuwa yakitoka kuanza safari zake nje ya geti la kuondokea mabasi ya mikoani
Basi linalofanya safari zake za Tanzania na Zimbabwe likitoka katika geti la stendi Ubungo kuanz safari zake…
Mmoja wa vijana wanaofaya shughuli zao ndani ya kituo cha mabasi ubungo, ‘Chalii’ ambaye pia ni mdau mkubwa wa kuperuzi habari za mtandao ukiwemo mtandao huu akiwa nje ya geti hilo akishuhudia mabasi hayo yaliyokuwa yakitoka baada ya mgomo kuisha.
Umati ukiendelea kushuhudia mabasi yaliyokuwa yakitoka mapema mchana wa leo Mei 5 baada ya mgomo kumalizika
“MWANAUME KAZINI’-Hali ya hewa ni baridi… lakini nilikuwa natokwa jasho baada ya kazi ngumu ya kutafuta picha za matukio kupitia kifaa changu kidogo yaani Pad ya Tecno P9, Namshukuru Mungu kwa hiki leo kwani hata huyo mwenye camera kubwa na mimi sote tumepata picha na siku zinaenda. !! Asante Mungu
Mwandishi Mwandamizi wa mtandao huu, Andrew Chale aki-Selfie’ na baadhi ya wadau wanaofanya shughuli zao katika kituo cha mabasi Ubungo muda mfupi baada ya mgomo kumalizika katika geti la kutokea magari yaendayo mikoani na nchi jirani.
Mwandishi Mwandamizi wa mtandao huu Andrew Chale akipiga ‘selfie’ huku akiwa ndani ya gari ndogo Cary ya 350gm, maarufu ‘Kilikuu’ akiondoka katika eneo la Ubungo kurejea na majukumu mengine ya kitaifa kufuatia kupiga kambi katika kituo hicho tokea asubuhi ya jana Mei 4 na kulala hapo hadi leo Mei 5, majira ya saa saba mchana anareje kwenye majumu mengine kufuatia kazi ngumu ya kuripoti mgomo huo.
Picha zaidi na habari zaidi za mgomo huu zitaendelea kuwajia hivi punde .. fuatana nasi, peruzi nasi kila siku kila saa. Tutaarifu na tutumie picha na habar 0719076376 au Whatsapp 0767076376