Quantcast
Channel: Uncategorized – DEWJIBLOG
Viewing all articles
Browse latest Browse all 5755

NIMR Mwanza wafanya mkutano wa wadau kuhusiana na madhara ya Pombe kwa vijana

$
0
0

tafiti

 

Na Andrew Chale wa Modewji blog

Taasisi ya  Taifa ya Utafiti ya Magonjwa ya Binadamu (NIMR)  tawi la Mwanza mapema  Machi 25 mwaka huu imeendesha warsha ya wadau mbalimbali kuhusiana na Madhara ya Pombe kwa vijana kufuatia utafiti uliofanywa katika maeneo kadhaa ya Tanzania, ikiwemo Mkoa wa Kilimanjaro.

Warsha hiyo iliwakutanisha wadau mbalimbali wakiwemo Madaktari,  wakuu wa idara za Polisi barabarani, wakuu wa Taasisi za Afya na mashirika ya kupiga vita matumizi ya vileo na wengineo.

Aidha kwa upande wake Dk. Said Kapiga kutoka NIMR Mwanza aliyetoa mada kwenye warsha hiyo, alisema licha ya wadau kupambana,  bado changamoto nyingi zinaikabili Nchi.

“Pombe inasababisha mambo mbalimbali ikiwemo magonjwa mengi zaidi  pamoja na hali ya utegemezi kwa jamii” alieleza Dk. Kapiga.

Dk. Ally Kapiga wa NIMR Mwanza akiongea na wandishi wa habari (hawapo pichani) kuzungumzia  mkutano huo wa wadau kuhusu madhara ya pombe kwa vijana

Dk. Ally Kapiga wa NIMR Mwanza akiongea na wandishi wa habari (hawapo pichani) kuzungumzia mkutano huo wa wadau kuhusu madhara ya pombe kwa vijana.

Pombe inasababisha kuenea kwa kasi pia ongezeko la magonjwa ya Ukimwi kwani,  mtu  anapolewa na kisha kujiingiza kwenye vitendo vya ngono ni rahisi kumpelekea vitendo vya kufanya tendo la ngono zembe.

Kwa upande wake, Dk. Ali Mzige alibainisha kuwa pombe pekee ina magonjwa mengi ikiwemo kansa na hata suala kukosa kizazi.

Katika hali nyingine, wadau hao walieleza kuwa, hadi sasa Serikali imeshindwa kushughulikia suala hilo matumizi ya Pombe ikiwemo kushindwa kushughulikia sera thabiti za kupunguza matumizi  ya pombe na tumbaku.

Kwa upande wake, baadhi ya wadau hao walienda mbali kwa kueleza kuwa, kwa sasa pombe za viroba ambazo zinapatikana kwa bei rahisi ni hatari kwani zimebainika kutengenezwa kwenye mazingira hatari.

Mkurugenzi Mtendaji wa Kliniki ya kimataifa ya afya ya uzazi kwa baba, mama, mtoto na vijana (AMM), Dk Ally Mzige  akitoa mada kwa wadau (hawapo pichani)

Mkurugenzi Mtendaji wa Kliniki ya kimataifa ya afya ya uzazi kwa baba, mama, mtoto na vijana (AMM), Dk. Ali Mzige akitoa mada kwa wadau (hawapo pichani).

“Kwa sasa pombe hizi za viroba  kuna maeneo huko Temeke imekutwa mitambo wakizitengeneza kwa kutumia dawa za kupuguza makali ya Virusi vya Ukimwi (ARV) na pia viroba vingine wanatengenezea kemikali za fomaling’.

Kwa upande wake, Mtaalamu wa NIMR Mwanza, Joel Francis alibainisha kuwa katika utafiti wao waliofanya maeneo kadhaa ikiwemo Mkoa wa Kilimanjaro, imebainika kuwa vijana wengi Mkoa huo wanatumia pombe.

Kwa upande wake, Dk. Ali Mzige alibainisha kuwa,  pombe zinazokaa kwenye paketi za ‘viroba’ humchukua mtu kulewa ndani ya dakika 6 hivyo pombe hizo ni hatari kwani zinaweza kukusababishia matatizo mengi ikiwemo ya kiafya.

Dk. Laetitia Sayi (Mtafiti binafsi-Freelance consultant) akijitambulisha kwenye mkutani huo wa wadau

Dk. Laetitia Sayi (Mtafiti binafsi-Freelance consultant) akijitambulisha kwenye mkutani huo wa wadau.

Viroba noma

Dk. Macca .A. Balwa kutoka Taasisi ya GIYEDOO inayopambana na masuala ya kupinga matumizi ya Pombe

Dk. Macca .A. Balwa kutoka Taasisi ya GIYEDOO inayopambana na masuala ya kupinga matumizi ya Pombe.

Dk Ally Mzige akiendelea na mada

Dk. Ali Mzige akiendelea na mada.

Dk. Praxeda Swai kutoka Muhimbili akijitambulisha kwenye mkutano huo

Dk. Praxeda Swai kutoka Muhimbili akijitambulisha kwenye mkutano huo.

Dk.Mariam Kalomo kutoka Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii (MoHSW)

Dk. Mariam Kalomo kutoka Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii (MoHSW).

Dk.Said Kapiga kutoka NIMR Mwanza,  akijitmbulisha kwenye mkutano huo wa  wadau  dhidi ya kupambana na Pombe kwa vijana mkutano uliofanyika jijini Dar es Salaam

Dk. Said Kapiga kutoka NIMR Mwanza, akijitambulisha kwenye mkutano huo wa wadau dhidi ya kupambana na Pombe kwa vijana mkutano uliofanyika jijini Dar es Salaam.

DSCN9863

Mkutano ukiendelelea.

Erick Moshi ambaye ni Afisa Mtawala  wa  Tanzania Public Health Asosiation (TPHA) akijitambulisha kwenye mkutani huo

Erick Moshi ambaye ni Afisa Mtawala wa Tanzania Public Health Asosiation (TPHA) akijitambulisha kwenye mkutani huo.

Florence .K. Francis  kutoka taasisi ya (F.I.T) DSM

Florence .K. Francis kutoka taasisi ya (F.I.T) DSM.

Haika Osaki wa NIMR Mwanza  akiwasilisha mada kwa wadau (hawapo pichani)

Haika Osaki wa NIMR Mwanza akiwasilisha mada kwa wadau (hawapo pichani).

Insp. Mossi .B. Ndozero kutoka makao makuu ya Kikosi cha Usalama Barabarani Nchini (TRAFFIC-HQ DSM)

Insp. Mossi .B. Ndozero kutoka makao makuu ya Kikosi cha Usalama Barabarani Nchini (TRAFFIC-HQ DSM).

Joel Msafiri wa NIMR Mwanza akitoa mada kwenye mkutano huo wa wadau

Joel Msafiri wa NIMR Mwanza akitoa mada kwenye mkutano huo wa wadau.

Mathias Herman mwakilishi kutoka UNESCO  akijitambulisha kwenye mkutano huo wa wadau( kushoto)

Mathias Herman mwakilishi kutoka UNESCO akijitambulisha kwenye mkutano huo wa wadau (kushoto).

Mkurugenzi wa TTCF. Lutgard Kagaruki (kushoto) akijitambulisha kwenye mkutano huo wa wadau

Mkurugenzi wa TTCF. Lutgard Kagaruki (kushoto) akijitambulisha kwenye mkutano huo wa wadau.

Mwandishi wa habari wa blog ya Jamii ya kutoka Michuzi Media Group kupitia blog ya Michuzi, Chalila Chibuda akijitambulisha kwenye mkutano huo wa wadau

Mwandishi wa habari wa blog ya Jamii ya kutoka Michuzi Media Group kupitia blog ya Michuzi, Chalila Chibuda akijitambulisha kwenye mkutano huo wa wadau.

Stafu wa NIMR tawi la Mwanza Haika Osaki akijitambulisha kwenye mkutano huo

Stafu wa NIMR tawi la Mwanza Haika Osaki akijitambulisha kwenye mkutano huo.

 

 


Viewing all articles
Browse latest Browse all 5755

Trending Articles