Quantcast
Channel: Uncategorized – DEWJIBLOG
Viewing all articles
Browse latest Browse all 5755

Abdulrahman Kinana: Wafuasi wa Chama cha CUF wako kifungoni

$
0
0

4

Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akizungumza na wana CCM wa maskani ya Mnarani Wilaya ya Micheweni na kuzungumza na wanachama wa maskani hiyo, Awali wakisoma taarifa yao mbele ya Katibu Mkuu wa CCM wanamaskani hao. Wamesema walihama kutoka Chama cha CUF na kujiunga na CCM lakini toka wamehama kutoka chama hicho wamekuwa wakinyanyaswa sana na kuzuiwa kufanya kazi ya uvuvi ikiwa ni pamoja na kutishiwa maisha na kuitwa makafiri na wafuasi wa CUF jambo ambalo linawasikitisha sana.

Kinana Akizungumza na vijana hao amesema Chama cha CUF hakitendi haki ya demokrasia kwani kila mtu kuhama au kuhamia katika chama fulani ni haki yake ya msingi kidemokrasia, lakini wanachama wa CUF wamekuwa kama wafungwa kwani hata kama hawakubaliana na baadhi ya mawazo ya viongozi wa chama hicho na Sera za chama hicho wanabaki kuvumilia na kuumia tu, jambo ambalo linawanyima demokrasia ya kweli ndani ya chama hicho.

Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana yuko katika ziara ya kikazi ya kisiwa cha Pemba akihimiza na kukagua utekelezaji wa ilani ya uchaguzi ya CCM ya mwaka 2010 ikiwa ni pamoja na kuhimiza uhai wa chama hicho kisiwani humo. (PICHA NA KIKOSIKAZI CHA FULLSHANGWE-MICHEWENI-PEMBA).

1020

Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana pamoja na viongozi wengine wakishiriki ujenzi wa tuta la kuzuia maji chumvi katika bonde la Mpunga la Koowe Wingwi Micheweni mkoa wa Kaskazini Pemba , kulia ni Vuai Ali Vuai Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar na kushoto ni Mkuu wa mkoa wa Kaskazini Pemba Ndugu Omar Khamis Othman.

11Balozi Ali Karume naye akishiriki katika ujenzi wa tuta hilo katikati ni Bw. Mbaruk Ali Mgau Afisa Imkuu Idara ya Umwagiliaji Mkoa wa Kaskazini Pemba. 12Moja ya malori yanayopeleka kifusi katika ujenzi wa tuta hilo likiwa limekwama kando ya tuta hilo 13Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akisalimiana na Dr.Rashid Daud Mkasha Mganga Mkuu wa Wilaya ya Micheweni mara baada ya kuwasili katika hospitali ya wilaya ya Micheweni wa pili kulia ni Dr. Omar Makame Khamis Daktari mdhamini wa hospitali hiyo. 14Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akipata maelezo kutoka kwa Dr.Rashid Daud Mkasha Mganga Mkuu wa Wilaya ya Micheweni wakati alipokuwa akikagua ukarabadi wa wodi katika hospitali hiyo. 15Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akishiriki ujenzi wa jengo la upasuaji katika hospitali ya wilaya ya Micheweni mkoa wa Kaskazini Pemba wanaoshuhudia ni madaktari viongozi mbalimbali wa wilaya ya Micheweni na hospitali hiyo.17Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiakimsikiliza Dr Omara Makame wakati akitoa maelezo b aada ya kutembelea na kukagua wodi na jengo la upasuaji.18Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiuliza jambo wakati alipokagua maabara ya hospitali hiyo kulia ni Fauz Abdi Nassor Ofisa viwango wa hospitaliya wilaya ya Micheweni.

1910

Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiwasili katika eneo la mkutano uwanja wa Majenzi Micheweni.

20Mjumbe wa kamati kuu ya CCM Ndugu Maua Daftari akizungumza na wananchi katika mkutano wa hadhara kwenye uwanja wa Majenzi Micheweni. 21Balozi Ali Karume naye akizungumza na wananchi katika mkiutano huo. 22Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiwa amekaa na viongozi mbalimbali meza kuu wakati wa mkutano huo. 23Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Ndugu Vuai Ali Vuai akizungumza katika mkutano huo. 24Baadhi ya wananchi wakiwa katika mkutano huo. 25

26

Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiwahutubia wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika kweny uwanja wa Majenzi mjini Micheweni. 27Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiwahutubia wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika kweny uwanja wa Majenzi mjini Micheweni. 28

29Viongozi hao wakiomba dua mara baada ya kumalizika mkutano huo.


Viewing all articles
Browse latest Browse all 5755

Trending Articles