Quantcast
Channel: Uncategorized – DEWJIBLOG
Viewing all articles
Browse latest Browse all 5755

Anayetuhumiwa kubaka watoto 11 kufikishwa mahakamani Hispania baada ya kusamehewa nchini Morocco.

$
0
0

Daniel-Galvan-detenido_MDSIMA20130806_0042_10

Maafisa nchini Hispania wamemkamata mwanamume anayetuhumiwa kuwanajisi watoto 11 walio kati ya umri wa miaka 4 na 15 nchini Morocco.

Mtu huyo  aliachiliwa hivi karibu baada ya kusamehewa na mfalme wa Morocco.

Daniel Galvan Vina (Pichani) anatarajiwa kufikishwa mbele ya mahakama kuu nchini Hispania.

Vina alikuwa akitumikia kifungo cha miaka 30 kabla ya mfalme Mohammed wa sita kumsamehe pamoja na wafungwa wengine 48 raia wa Hispania wiki iliyopita.

Taarifa za kuachiliwa kwake zilizua maandamano makubwa yaliyoambatana na ghasia nchini Morocco na kumlazimu mfalme huyo kubatilisha uamuzi wake.

Inadaiwa  mfalme Mohammed  hakufahamu ukubwa wa kosa alilofanya raia huyo mhispania wakati akitoa amri hiyo ya kumsamehe yeye pamoja na wenzake.


Viewing all articles
Browse latest Browse all 5755

Trending Articles