Quantcast
Channel: Uncategorized – DEWJIBLOG
Viewing all articles
Browse latest Browse all 5755

Makabidhiano ya Ofisi kati ya Waziri Dkt. Mwinyi na Dkt. Seif

$
0
0

DSC_1613

Aliyekuwa Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii na sasa ni Waziri wa Ulinzi na jeshi la Kujenga Taifa, Dkt. Hussein Mwinyi (kushoto) akizungumza  na watendaji wa wizara hiyo (hawapo pichani) wakati wa makabidhiano ya ofisi  na aliyekuwa Naibu Waziri wake na sasa ameteulikuwa kushika nyadhifa ya Uwaziri Dkt. Seif Rashid (kulia), anayefuata ni Naibu Waziri wa  Wizara hiyo Dkt. Kebwe S. Kebwe.Makabidhiano hayo yamefanyika kwenye ukumbi wa Waziri, wizarani hapo.

DSC_1645

Waziri wa  Afya na Ustawi wa jamii Dkt. Seif Rashid (kulia) akizungumza na watendaji wa wizara hiyo (hawapo pichani) na kutoa shukrani zake za dhati kwa aliyekuwa Waziri wake Dkt. Mwinyi  kwa ushirikiano wake kipindi alipokuwa akiongoza wizara hiyo.

DSC_1660

Naibu Waziri  Dkt. Kebwe S. Kebwe akizungumza na watendaji wa wizara hiyo na kuwataka kufanya kazi kwa ushirikiano na mahusiano mazuri  ili kukabiliana na changamoto zinazoikabili sekta hiyo.

DSC_1661

Waziri wa Ulinzi Dkt. Mwinyi akiteta jambo na katibu Mkuu wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jami, Charles Pallangyo.

DSC_1670

Mawaziri hao wakisaini vitabu vya makabidhiano ya Muundo na Utekelezaji wa Wizara.

DSC_1677

Aliyekuwa Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dkt. Mwinyi akimkabidhi kitabu hicho Waziri Mpya wa Wizara hiyo Dkt. Seif.

DSC_1680

Naibu Waziri Dkt. Kebwe, akikabidhiwa  kitabu na Waziri Dkt. Mwinyi.

DSC_1693

Mawaziri hao wakiwa kwenye picha ya pamoja mara baada ya makabidhiano pamoja na watendaji wa wizara hiyo. Wa kwanza kushopto waliokaa ni Katibu Mkuu, Charles Pallangyo, aliyekuwa Waziri wa afya na ustawi wa jamii Dkt. Mwinyi, Waziri mpya wa wizara hiyo Dkt. Seif nna wa mwisho kulia ni Naibu Waziri Dkt. Kebwe S. Kebwe ( Picha zote na Catherine Sungura-MOHSW).
 


Viewing all articles
Browse latest Browse all 5755

Trending Articles