Quantcast
Channel: Uncategorized – DEWJIBLOG
Viewing all articles
Browse latest Browse all 5755

Ajali 3 zatokea leo Nchini: Ya Ruaha Mbuyuni 18 wadaiwa kupoteza maisha

$
0
0

unnamed (67)

Mabaki ya ajali iliyotokea maapema asubuhi ya leo inayoelezwa kuuwa watu 18 na kujeruhi 10 huko Ruaha Mbuyuni.

Na Andrew Chale wa Modewji blog

Hadi tunaendelea kuwapatia taarifa hizi usiku huu, tayari imeelezwa kuwa zaidi ya abiria 18, wameripotiwa kupoteza maisha huku 10 wakijeruhiwa vibaya katika ajali ya gari iliyotokea mapema leo majira ya asubuhi iliyohusisha basi la Abiria la Nganga lililogongana na lori aina ya Fuso uso kwa uso, hali iliyopelekea kuungua  kwa magari hayo.

Awali taarifa kutoka eneo la tukio  majira ya saa Nane  mchana tuliripoti waliopoteza maisha ni abiria 6, lakini kwa sasa idadi hiyo imeelezwa kuongezeka na kwa sasa VIFO ni 18  huku zaidi ya 10 wakijeruhiwa vibaya Hii ni wa ajali iliyotokea mpakani mwa Morogoro na Iringa. TAARIFA ZAIDI TUTAENDELEA KUWAJUZA KADRI TUTAKAVYOZIPATA 0719076376/ Whatsapp0767076376.

           Ajali Dodoma majira ya jioni ‘vifo zaidi kuripotiwa’

11138116_548742381934581_9197825229175766682_n

 Gari aina ya Fuso lililokuwa limepakia watu kutoka msibani likionekana kuharibika vibaya baada ya kugongana naa kontena.

Habari zilizotufikia kwenye chumba chetu cha  habari cha Modewji blog ni kuwa kuna ajaali mbaaya imeweza kutokea maeneo ya Ngilori na Tabu hotel  huko Wilayani Gairo, Dodoma.  Imeelezwa kuwa, ajali hiyo imehusisha lori aina ya Fuso iliyokuwa imepakia watu waliotoka msibani na gari kubwa aina ya semi trera na kugongana  uso kwa uso.

lori

Lori hilo linavyoonekana huku pembeni baadhi ya wananchi wakiangalia miili na majeruhi muda mfupi baad ya kufanya msaada huko Gairo, Dodoma jioni ya leo Aprili 12.

Hata hivyo, Idadi kamili ya watu waliopoteza maisha bado haijapatikana ila waliokaribu na tukio hilo wanaelezea kuwa ni ajali mbaya sana  huenda vifo vikawa vingi zaidi hii ni taarifa ya Gairo, Dodoma  kwa habari zaidi tutaendelea kukufikishia hapa.

Zaidi ya abiria 50 wanusurika kifo..basi lao lagongana uso kwa uso na lori la mafuta huko Tanga jioni ya leo

unnamed (9)Basi la Burudani likionekana mara baada ya ajali hiyo kutokea huko eneo la Soni, jimbo la Bumbuli Mkoani Tanga.

Habari ambazo zimeweza kupatikana ni kuwa zaidi ya abiria 50 wamenusurika kifo baada ya basi lao lililojulikana kwa jina la Burudani,  kugongana uso kwa uso na Lori la tenki la mafuta maeneo ya Soni  katika jimbo la Bumbuli, mkoani Tanga.

Kwa mujibu wa taarifa hizo ni kuwa, ilielezwa kuwa  Lori la mafuta lilikata breki na kuvaana na basi hilo uso kwa uso. Kwenye ajali hiyo haakuna kifo ila inaelezwa kuwa abiruiiaa kadhaa wamejeruhiwa na wamekimbizwa Hospitali. Tutaendelea kukuletea taarifa zaidi kila zinapopatikana kutoka vyanzo mbali mbali vya habari popote pale  na kukujuza hapa zikiwa zimehaririwa na kukufikishia wewe msomaji wetu. 

Asante endelea kuwa nasi, endelea kuperuzi nasi kila saa kila wakati.


Viewing all articles
Browse latest Browse all 5755

Trending Articles