Quantcast
Channel: Uncategorized – DEWJIBLOG
Viewing all articles
Browse latest Browse all 5755

Mwakilishi Jimbo la Bububu Mhe BHAA akanusha tuhuma ya gari lake kuhusika mashambulizi dhidi ya Wanachama wa CUF

$
0
0

Mwakilishi wa Jimbo la Bububu Zanzibar Mhe Hussein Ibrahim Makungu akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na tuhuma zanazoenezwa kwamba gari lake aina ya fuso kuhusika na kuwashambulia Wanachama wa CUF wakati wakirudi Mkutanoni makunduchi, Akitowa maelezo kwa waandishi wa habari katika ukumbi wa salama bwawani amesema gari hiyo iliotumika katika tukio hilo haiko katika milki yake, hiyo gari iliohusisha na tukio hilo aliiuzwa karibu sasa miaka minane na kumulikiwa na mtu mwengine akiwa bado hajalifuta jina la Bhaa Staily,

Amesema analaani kitendo hicho waliofanyiwa wananchi hao.

Mhe. Hussein Ibrahim Makungu, akisisitiza jambo wakati wa mkutano huo na kusema gari lajimbo siku hiyo halikutoka kwenda popote na kuegeshwa katika hospitali ya Kibweni KMKM, anashangaa kusikia kauli hiyo ya kulihusisha gari hilo na tukio na kueleza kwa waandishi wa wahabari Zanzibar

Waandishi wakifuatilia kwa makini mazungumzo ya mkutano huo na Mhe Hussein Ibrahim Makungu BHAA.katika ukumbi mdogo wa salama bwawani Zanzibar.

Waandishi wakifuatilia kwa makini mazungumzo ya mkutano huo na Mhe Hussein Ibrahim Makungu BHAA.katika ukumbi mdogo wa salama bwawani Zanzibar.


Viewing all articles
Browse latest Browse all 5755

Trending Articles