Mmoja wa kundi la Wananchi waliovunjiwa nyumba zao kupisha ujenzi wa Chuo cha Afya cha Muhimbili (MUHANS) akifafanua jambo kwa waandishi wa habari ambae hakutaka jina lake litajwe ambapo alisema “ Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Dk, Shukuru Kawambwa ameamua kutukimbia wakati anajua wazi kuwa tumekuja hapa ili atutatulie kero zetu lakini yeye anaamua kutokea mlango wa nyuma hivi kweli tunajenga taifa la namna gani kama waziri mwenye dahamana uaaogopa wananchi wake kuwapa ukweli”. Ambapo pia aliongeza kuwa mwezi wa Saba mwaka jana walilazimishwa kuvunjiwa nyumba zao bila kupewa taarifa mapema hatua iliyowafanya kwenda kwa Mkuu wa Mkoa ili kupatiwa ufumbuzi wa tatizo lao lakini mpaka hii leo bado hawajapatiwa maelezo ya kueleweka zaidi ya kuzungushwa kila kukicha.
Aliongeza kuwa “ Ndugu Mwandishi sisi kama unavyotuona hapa toka asubuhi tupo hapa kwanza tuliambiwa twende Wizarani tulipofika Wizarani tukaambiwa Waziri hayupo ameenda katika mkutano huko viwanja vya Gymkhana na ndipo tukaamua kuja kumuona lakini mpaka sasa hatumuoni huyo Waziri”, alisema.
Mkazi wa jiji la Dar Maria Daudi akilia kwa uchungu huku akisaidiwa na wasamaria wema nje ya ukumbi wa mwalimu Nyerere jijini Dar es salaam, Lengo la Maria ni kumtaka Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Dk, Shukuru Kawambwa atoke ili kumueleza shida yake, ambapo nyumba yake ilivunjwa kupisha ujenzi wa chuo cha Afya cha Muhimbili (MUHANS) huko Kibamba –Mlonganzilo.
Maria Daudi akigaragara chini huku msamaria mwema akijaribu kumbembeleza na kumwinua.
Mmoja wa wananchi hao akionyesha moja ya nakala walizokabidhiwa ili kupatiwa malipo yao.
Palikuwa hapatoshi full vilio.(PICHA NA PHILEMON SOLOMON WA FULLSHANGWE DAR ES SALAAM).