Quantcast
Channel: Uncategorized – DEWJIBLOG
Viewing all articles
Browse latest Browse all 5755

Mkombozi Benki kusomesha yatima

$
0
0

1

Mkurugenzi Mtendaji wa Benki Mkombozi Commercial, Edwina Lupembe.

Na Mwandishi wetu

Benki ya Mkombozi nchini imesema kuwa mchango wa kifedha  wanazopata  katika  shughuli za kijamii  umekuwa  wakimafanikio  makubwa  hasa  kupitia  uwekezaji wa sekta ya  elimu  Nchini, kwani  hali  hiyo  inachangia  kwa  kasi  maendeleo  ya Taifa kwa kuwa  na  wataalamu wa Nyanja  mbalimbali wenye  uwezo  mkubwa.

Taasisi  za kifeda  kama  mabenki   wamekuwa ni  wadau  wakubwa  wa mchango  huo,  hivi  karibuni  benki  ya  mkombozi  Tanzania  inayomilikiwa  na baraza  la  Maaskofu Tanzania (TEC)imejikita  katika  kuisaidia  jamii  kielmu  kupitia   kuwasaidia  watoto  yatima  kwa  kuwawezesha  kielimu  kupitia  kugharamikia masomo  yao.

Kituo  cha watoto  yatima cha  kijiji cha  matumaini(Village  of Hope), kata  ta Mkolani, Wilaya  ya   Nyamagana  Jijini Mwanza,  kwa kuwasaidia  watoto  wao kuwasomesha  masomo  ya Sekondari hadi   kidato  cha  sita (6).

Akiongea  mbele  ya  vyombo   vya  habari  meneja  wa  benki  ya  Mkombozi Jijini Mwanza  kwa niaba  ya  mkurugenzi  mtendaji wa benki  hiyo  bwana  Nichorus  ,  Nicholas   Mokirya   alisema  kuwa  wamekuwa  na  utaratibu wa kurudisha  faida wanayoipata  kwa jamii  kupitia   uwekezaji  katika  Nyanja ya  kielimu.

Bwana Nichorus  aliongeza kuwa  wameamua  kuwasaidia  watoto watatu  toka  kituo  hicho  cha  watoto yataima ambao  ni Nancy  Oscar  mwanafunzi wa kidato cha  tatu,           wa  pili  ni  Kashuliza  Kamugisha  kidato  cha  pili,  na  wa  mwisho  ni  Peter  Aklan  anasoma  kidato  cha  kwanza .wanafunzi  hawa  wanasoma  shule  ya  sekondari  ya  Twihulumile iliyopo  kata  ya  Butimba  wilaya  ya  nyamagana  wanaishi  katika  kituo  cha kijiji  cha  matumaini  nyegezi Mwanza  .

Watoto  hao wote watatu  wamekuwa  wakifanya  vyema katika  masomo yao  hali ilioyowavutia  benki  ya Mkombozi  kutoa   msaada  wa kielimu  kuwasomesha  wanafunzi hao  hadi  kiwango  cha  kidato  cha sita.

“Tuna amini kuwa  jamii  yoyote ile  ili iweze  kuendelea  lazima  iwekeze  kwenye elimu, hivyo basi  sisi  tumeamua  kuwekeza kwa  watanzania   kwa  kuwapa  msaada   kielimu  kwani  tuna amini  kuwa  jambo  hili  litakuwa la  faida  kwa jamii  nzima  na wala hatutajuta  kwa  uamuzi  wetu   huo, tunachokiomba  ni juhudi zao  watoto  wote  wanaowezeshwa  na benki yetu katika  kupata  elimu   ili waweze  kutimiza    ndoto zao”.

Jambo hilo  lililofanywa na benki  hiyo  ni la  mzingi sana  kwani  hata  sera  ya  elimu  ya mwaka  1995  inasisitiza  kuwaendeleza  wanafunzi    na kuwatayarisha  kikamilifu  katika  ngazi  ya  sekondari ili waweze  kuja  kuwa  wataalumu wenye ujuzi  katika ngazi  za vyuo  vya  ufundi  na  vyuo vikuu. 

Benki  ya biashara  ya  mkombozi  ilianza  rasmi  28 Agosti   28, 2009  ikiwa  na  matawi  manne  matatu  yako Dare es salaam  na  moja  liko  katika  mkoa  wa  Mwanza, ambayo  yanatoa  huduma  zote za kibenki   na  kuchochea  maendeleo  katika  mfumo wa sayansi  na teknolojia.

Kwa  kuona  umuhimu  wa kuisadia  jamii, benki  hiyo  iliweza  kuisadia  jamii   iliyokumbwa  na  uyatima  kwa  kuwasomesha  watoto  watatu   mwaka  2013  kutoka  Jijini  Dar  es Salamu  kwa kuwagaharamikia  masomo  yao  sanjali  na   mwaka 2014  ilipoendeleza  sera  yake kwa kuwasaidia  watoto  wengine  watatu   toka Jijini Mwanza.

“Kwa  upoande wangu  mimi  nawashukuru sana  benki  ya  Mkombozi  kwa kutusaidia, kwani  naona sasa  ndoto  zangu za  kuja  kuwa  Daktari  zinatimia  hasa  leo  nilipopata  ufadhili  huu wa  masomo  yangu, kwani  sina  ndugu wenye uwezo  wa kunisaidia”. Alisema  mwanafunzi  Nancy  Oscar  wa kidato  cha  tatu   anayesoma  shule  ya  Sekondari  ya Twihurumile  kata  ya Butima, Wilaya  ya  Nyamagana Jijini Mwanza  mchepuo  za  sayansi.

Naye  mwanafunzi   mwingine  Peter Aklani  anayesoma  kidato  cha  kwanza, mwenye  ndoto z akuja  kuwa  injinia  aliishukuru sana  benki  hiyo    kwa kumsaidia  na kuiomba iendelee  kutoa  elimu  zaidi  kwa  watoto  wengine  yatima  wasio  kuwa na msaada ili  waweze kukamlisha  ndoto zao.

Ni wazi  kuwa  wewe  msomaji wa makala  hii  unakumbuka  kuwa  Nchi  yetu  ya Tanzania  imekuwa  mstari wa mbele  katika kuhakikisha  kila  mtanzania  anapata  elimu  bora  kupitia  mipango na mikakati mbalimbali  ikiwemo  ile  ya malengo  ya  milleninia  yanayotekelezwa na  mpango  wa MKUKUTA  ili  kufika  mwaka 2015  basi  Tanznaia  iwe  imepiga hatua  kubwa  ya maendeleo.

Kilichofanywa  na benki ya Mkombozi  ni mfano wa kuigwa kwa  taasisi nyingine  za kifedha  hapa  Nchini,  kwani    uwekezaji wa kilelimu  ndiyo uwekezaji  nambari  moja  kwa  Nchi  iliyo  makini  inayotaka  kuendelea, ni mifano mingi  tu  inayotukumbusha  mbali  mfano  wa  zile  Nchi za bara  la  Asia, ambapo miaka  ya  1970  na 1980  tulikuwa  katika  mstari  mmoja wa maendeleo lakini leo  hii  wenzetu  wametuacha  mbali sana, kwa kuwa  walithubutu  kuwekeza katika  Nyanja  ya  elimu. Ongereni sana Mkombozi  kwa  kutumia  jicho  la  tatu  kuona mbali  na kuamua  kuipa  kipaumbele  cha  kwanza  elimu  hasa  kwa watoto  wetu  mayatima, huo ni mfano wa kuigwa.


Viewing all articles
Browse latest Browse all 5755

Trending Articles