Quantcast
Channel: Uncategorized – DEWJIBLOG
Viewing all articles
Browse latest Browse all 5755

Mamlaka ya usafiri wa anga yadhamini kongamano la mafunzo ya mfumo mpya wa shirika la kimataifa la usafiri wa anga – ICAO

$
0
0

05

Kaimu Mkurugenzi  Mkuu wa Mamlaka ya usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) Charles Chacha(kushoto) akiongea wakati wa uzinduzi wa kongamano la mafunzo ya mfumo mpya wa shirika la Kimataifa la usafiri wa Anga (ICAO) lenye kulenga ufanisi wa wataalamu wa kuongoza ndege vyombo vya usafiri wa anga pamoja na mitambo ya kuongonzea ndege. katikati ni Meneja mratibu wa safari za ndege Afrika Frederic Legrand, Kongamano hilo linazihusisha nchi za Afrika linafanyika hapa nchini kwa  siku tatu kuanzia leo katika hateli ya Serena jijini Dar es Salaam. Kaimu Mkurugenzi Idara ya Huduma za Uongozaji ndege Said Onga (Kulia).

06

03

Afisa wa Kanda ya Afrika wa  ICAO  Papa Issa Mbengue (kushoto)akisisitiza jambo juu ya mfumo mpya wa shirika la Kimataifa la usafiri wa Anga (ICAO) lenye kulenga ufanisi wa wataalamu wa kuongoza ndege, vyombo vya usafiri wa anga pamoja na mitambo ya kuongonzea ndege wakati wa Kongamano la mafunzo ya ufanisi wa masuala ya uongozaji wa ndege linalofanyika kwa siku tatu katika hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam kwa udhamini wa Mamlaka ya usafiri wa Anga Tanzania (TCAA)  wanaomsikiliza ni  Kaimu Mkurugenzi  Mkuu wa Mamlaka ya usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) Charles Chacha (watatu kutoka kulia) Kaimu Mkurugenzi Idara ya Huduma za Uongozaji ndege Said Onga (Kulia) Meneja mratibu wa safari za ndege Afrika Frederic Legrand. (wapilia kutoka kulia) na Makamu wa rais wa airspace and airlines Servises Airbus ya Ufaransa Don Facpues  Ould.

08

Kaimu Mkurugenzi  Mkuu wa Mamlaka ya usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) Charles Chacha akimsikiliza kwa makini Meneja mratibu wa safari za ndege Afrika Frederic Legrand(African Flight Proceducare Manager) wakati alipokuwa akizungumza kwenye  kongamano la mafunzo ya mfumo mpya wa shirika la Kimataifa la usafiri wa Anga (ICAO) lenye ufanisi wa wataalamu wa kuongoza ndege ,vyombo vya usafiri wa anga pamoja na mitambo ya kuongonzea ndege.Kongamano hilo la siku tatu  katika hateli ya Serena jijini Dar es Salaam  kwa udhamini.

09

Baadhi ya washiriki wa kongamano la mafunzo ya mfumo mpya wa shirika la Kimataifa la usafiri wa Anga (ICAO) lenye ufanisi wa wataalamu wa kuongoza ndege ,vyombo vya usafiri wa anga pamoja na mitambo ya kuongonzea ndege,wakifuatilia moja ya mada zilizokuwa zikitolewa hapo  kongamano hilo limedhaminiwa na TCAA.

10

Kaimu Mkurugenzi  Mkuu wa Mamlaka ya usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) Charles Chacha akisalimiana na baadhi ya washiriki wa kongamano la mafunzo ya mfumo mpya wa shirika la Kimataifa la usafiri wa Anga (ICAO) lenye ufanisi wa wataalamu wa kuongoza ndege ,vyombo vya usafiri wa anga pamoja na mitambo ya kuongonzea ndege,wakifuatilia moja ya mada zilizokuwa zikitolewa hapo  kongamano hilo limedhaminiwa na TCAA linalofanyika kwa siku tatu kuanzia leo katika hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam.

02

Washiriki wa kongamano la mafunzo ya  mfumo mpya wa shirika la kimataifa la usafiri wa anga (ICAO)kutoka nchi za Nigeria, Mali, Ivory coast, Senagal, Rwanda, Cape Verde, Gabon na Tanzania wakiwa katika picha ya pamoja wakati wa Kongamano hilo la siku tatu linalofanyika kwenye hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam.

01

Kaimu Mkurugenzi  Mkuu wa Mamlaka ya usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) Charles Chacha (kulia) akisalimiana na  Makamu wa rais wa airspace and Airlines Servises Airbus ya Ufaransa Don Facpues  Ould, baada ya kufungua kongamano la mafunzo ya mfumo mpya wa shirika la Kimataifa la usafiri wa Anga (ICAO) lenye ufanisi wa kulenga wataalamu wa kuongoza ndege ,vyombo vya usafiri wa anga pamoja na mitambo ya kuongozea ndege. Kongamano hilo linafanyika kwa siku tatu kuanzia leo katika hateli ya Serena jijini Dar es Salaam.Katikati ni Meneja mratibu wa safari za ndege Afrika Frederic Legrand.(African Flight Proceducare Manager)


Viewing all articles
Browse latest Browse all 5755

Trending Articles