Mkurugenzi mtendaji wa TDL David Mgwasa akielezea na kutoa ufafanuzi wa Kinywaji kipya aina ya Fyfe’s.Kampuni ya Tanzania distilleries ltd (tdl) Juzi Tarehe 20 mwezi wa 8 2014 imefanya uzinduzi wa kinywaji chake kipaya aina ya Fyfe’s katika hoteli ya Serena, Kinywaji hicho ambacho uhalisia wake na uzindikaji ni wa nchini scotland.Mkurugenzi wa TDL David Mgwasa amewaomba waTanzania kukipokea kinywaji hicho kwenye soko la vimiminika kwani kina ubora wa hali ya juu na kimetengenezwa kwa asilimia kubwa kwa kutumia vitu asilia.
Langas Group wakiingia ukumbuni kwa kutoa burudani ikiwa ni kumkaribisha Bwana Langa Khanyile ambaye ni mtaalamu wa masuala ya upishi wa bia na uchanganyaji.
Langa Khanyile mtaalamu wa upikaji na uchanganyaji wa kinywaji cha Fyfe’s akicheza kwa furaha na mshehereshaji wa shughuli hiyo Jimmy Kabwe ndani ya Serena Hotel wakati wa uzinduzi huo.