Quantcast
Channel: Uncategorized – DEWJIBLOG
Viewing all articles
Browse latest Browse all 5755

Rais wa Nigeria akutana na rais Jinping wa China katika mazungumzo ya kuimarisha mahusiano ya kiuchumi.

$
0
0

628x471

 

Rais Goodluck Jonathan wa Nigeria amekutana na rais Xi Jinping wa China mjini Beijing, katika ziara yake inayolenga kuimarisha uhusiano wa kibiashara kati ya nchi hizo mbili.

Rais Jonathan ambaye amefuatana na maafisa 19 wa ngazi ya juu wa serikali yake, amesema China ina uchumi imara na kwamba kampuni za nchi hiyo zinaendelea na mradi wa ujenzi wa barabara nchini Nigeria, wenye thamani ya dola bilioni 1.7.

Wakati wa mkutano huo, mikataba mitano ilisainiwa ikiwemo ya masuala ya kibiashara, kanuni za visa, kiufundi na masuala ya kisheria yanayohusisha kuuza na kununua bidhaa za kiutamaduni.

China ambayo ina uchumi mkubwa barani Asia, imeonyesha nia ya kutaka kuongeza maslahi zaidi katika sekta ya mafuta Nigeria, nchi ambayo inaongoza kwa kuuza mafuta barani Afrika.


Viewing all articles
Browse latest Browse all 5755

Trending Articles