Afisa Elimu Msingi wilaya Sengerema Bw. Juma Mwajombe akikadhiwa madawati.
Na Daniel makaka, Sengerema.
WALIMU wakuu shule za msingi katika kata ya Bupandwa wilaya ya Sengerema mkoa wa Mwanza wameombwa kutumia vyema madawati yaliyotolewa na uongozi wa msitu wa Buhindi kwa lengo la kusaidia kutatua tatizo la madawati katika shule hizo.
Hayo yamesemwa na Afisa Elimu ya msingi wilaya ya Sengerema Bw Juma Mwajombe katika sherehe za kukabidhiwa madawati hayo iliyofanyika katika sherehe za Mei Mosi katika kata ya Bupandwa ambapo uongozi wa msitu wa Buhindi ulikabidhi madawati 80 katika kata hiyo ambapo yatagawiwa katika shule zote za kata hiyo .
Diwani wa kata ya Bupandwa Bw. Masumbuko Bupamba akitoa shukurani baaada ya kukabidhiwa madawati.
Akikabidhi madawati hayo Meneja Msaidizi wa Msitu huo Bw Ernesti Madatta amesema kuwa msitu wa Buhindi umekuwa mstari wa mbele kusaidia jamii hiyo na itaendelea kutoa misaada katika shule hizo ili kuleta usawa kwa kuwa jamii hiyo inasaidia kulinda raslimali za msitu huo.
“madwati haya yamegharimu zaidi ya shilingi za kitanzania milioni tatu fedha taslimu na tutaendelea kutoa msaada kwenye jamii zinazotuzunguka,’ amesema Madatta.
Meneja msaidizi msitu Buhindi Bw. ERNEST MADATA.
Bw, Madata aliongeza kuwa sambamba na kukabidhi madawati hayo pia msitu huo unajenga kituo cha afya katika kata hiyo pia jengo la mama na mtoto katika zahanati ya Bupandwa ambapo kila moja itagharimu shilingi milioni sabini pia amewataka wananchi wa kata hiyo kushirikiana vema na msitu huo kuleta ushirikiano wa dhati miongoni mwao.
Kwa upande wake Diwani wa kata hiyo Bw Masumbuko Bupamba amemshukuru meneja huyo jinsi wanavyosaidia jamii hiyo na amewaomba waendelee na juhudi hizo za kusaidia jamii.
Msitu wa Buhindi.