Mhandisi Mkazi Eng. Peter Gibson (aliyenyoosha mkono) kutoka Kampuni ya Nicholas O’ Dwyer & Partner akimpatia maelezo Waziri wa Ujenzi Mhe. John Pombe Magufuli, kuhusu utekelezaji wa ujenzi wa mradi wa barabara ya Mbeya – Chunya. Kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Mhe. Abbas Kandoro.
Waziri Wa Ujenzi Mhe. John Pombe Magufuli (katikati aliyeinama) akiangalia mamendeleo ya ujenzi wa barabara ya Mbeya – Chunya. Kushoto kwa Waziri Magufuli ni Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Mhe. Abbas Kandoro.
Waziri Wa Ujenzi Mhe. John Pombe Magufuli (aliyetangulia) akikagua mamendeleo ya ujenzi wa barabara ya Mbeya – Chunya. Nyuma ya Waziri Magufuli ni Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Mhe. Abbas Kandolo.
Mhandisi Mkazi Eng. Peter Gibson (kushoto) kutoka Kampuni ya Nicholas O’ Dwyer & Partner akimpatia maelezo Waziri wa Ujenzi Mhe. John Pombe Magufuli, kuhusu uwekaji wa lami katika barabara ya Mbeya – Chunya sehemu kati ya Lwanjilo na Chunya.
Mkandarasi aliyekuwa amepewa kazi ya kujenga barabara ya kuanzia Mbeya mjini hadi Lwanjilo kwa kiwango cha lami anatakiwa kuilipa Serikali ya Tanzania Shilingi bilioni 16 baada ya kushindwa kesi. Kampuni ya Kundan Singh ya kutoka Kenya iliachakazi za ujenzi kinyume na mkataba na kukimbilia mahakamani ambako imeshindwa na kutakiwa kulipa kiasi hicho cha fedha.
Kuchelewa kukamilika kwa mradi wa ujenzi wa barabara kati ya Mbeya na Chunya kumekuwa kukilalamikiwa kwa kipindi kirefu. Hivyo kupatikana kwa mkandarasi wa kumalizia kazi kwa sehemu ya kwanza kumeleta faraja kubwa kwa wananchi wa maeneo hayo ambao wengi wao waliitikia vyema wito wa kubomoa majengo yao yaliyo ndani ya hifadhi ya barabara ili kupisha ujenzi mradi huo.