Makamu wa Rais Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akimuelekeza jambo Dkt. Vidast Makota Mkurugenzi Habari Uenezi na Mawasiliano wa Baraza la Taifa la Kuhifadhi Mazingira (NEMC) alipotelea mabanda ya maonesho katika maadhimisho ya siku ya Mazingira Duniani yaliyofanyika katika kijiji cha Namanyere Wilayani Nkasi Nkoani Rukwa.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungnao wa Tanzania Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiwasha mashine kuzindua pampu ya maji kwa wananchi wa mji wa Namanyere Wilayani Nkasi, katika kilele cha Maadhimisho ya siku ya Mazingira Duniani, ambapo hapa Nchini yameadhimishwa rasmi Mkoani Rukwa. Wa pili kulia Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira Dkt. Terezya Huvisa.
Makamu wa Rais Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiangalia vijarida mbalimbali alipotembelea Banda la Ofisi ya Makamu wa Rais katika maonesho ya maadhimisho ya siku ya Mazingira Duniani yaliyofanyika katika viwanja vya sabasaba Namanyere Wilayani Nkasi Mkoani Rukwa, kulia Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira Dkt. Terezya Huvisa.
Makamu wa Rais Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akitembelea mabanda ya maonesho kwenye maadhimisho ya siku ya mazingira Duniani yaliyoadhimishwa katika Viwanja vya sabasaba kijiji Namanyere Wilayani Nkasi Mkoani Rukwa.
Makamu wa Rais Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiangalia baadhi ya miche ya mimea katika banda la Asasi ya Vijana wa kuhifadhi Mazingira Rukwa alipotembelea maonesho kwenye maadhimisho ya siku ya mazingira Duniani yaliyoadhimishwa Kitaifa jana katika Viwanja vya sabasaba Namanyere Wilayani Nkasi Mkoani Rukwa.
Makamu wa Rais Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akikabidhi kikombe kwa Meya wa Manispaa ya jiji la Mwanza Stanlaus Mabula ambapo Halmashauri ya jiji la Nyamagana Mwanza imeibuka Mshindi katika mashindano ya utunzaji wa Afya kwenye maadhimisho ya siku ya mazingira Duniani yaliyoadhimishwa Kitaifa katika Viwanja vya sabasaba Namanyere Wilayani Nkasi Mkoani Rukwa.
Makamu wa Rais Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akihutubia Wananchi kwenye maadhimisho ya siku ya mazingira Duniani yaliyoadhimishwa Kitaifa katika Viwanja vya sabasaba Namanyere Wilayani Nkasi Mkoani Rukwa.
Kikundi cha Taarab cha TOT chini ya uongozi wa Malkia wa Mipasho Hadija Omar Kopa kikitumbuiza kwenye maadhimisho ya siku ya Mazingira Duniani Kitaifa yaliyoaadhimishwa katika viwanja vya sabasaba Wilayani Nkasi Mkoani Rukwa. Wa kwanza kushoto anaejirusha ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira Dkt. Terezya Huvisa. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais).